TAARIFA KWA UMMA JUU YA KUHAMIA JENGO LA ZBS, MARUHUBI.
Zanzibar, 20 Mei, 2022.
Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) yenye Makao Makuu yake Amani
viwanda vidogo vidogo na Malindi Mjini Unguja katika kuboresha
utendaji wake inapenda kuwajuulisha wananchi wote na wadau
wake kua ofisi hizo zilizopo Amani na malindi zinahama na kuhamia
katika jengo lao jipya liliopo Maruhubi nyuma ya eneo la Afisi za
uchapaji.
Hivyo kuanzia tarehe 1/06/2022 huduma zote zilizokua zinapatikana
katika ofisi zao hizo za (Amani na Malindi) zitatolewa rasmi katika
ofisi yao mpya iliopo Maruhubi.
Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Ahsante.
Imetolewa na:
KITENGO CHA UHUSIANO
TAASISI YA VIWANGO ZANZIBAR
S.L.P 1136
ZANZIBAR